TAFUTA CHOCHOTE NDANI YA NKEMA

Friday 31 October 2014

Serikali isikwepe kulipa malimbikizo ya madeni MSD kuokoa maisha ya Watanzania!

Taarifa kwa Vyombo Vya Habari, 30 Octoba 2014

Serikali isikwepe kulipa malimbikizo ya madeni MSD kuokoa maisha ya Watanzania!

Sikika imesikitishwa na tamko lililotolewa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, kuhusiana na kushindwa kwa vituo vya huduma za afya kununua dawa MSD kutokana na kuongezeka kwa deni. Ni wazi kuwa waziri hajalipa tatizo hili uzito unaotakiwa na kutambua kuwa baadhi ya wagonjwa wanaweza kupoteza maisha kutokana na tatizo hili.

Sikika inatambua kuwa, mapato yatokanayo na uchangiaji katika huduma za afya ni moja tu ya vyanzo vinavyotumika katika kuongeza upatikanaji wa dawa na vifaa tiba nchini. Na pia inatambua kuwa chanzo hiki pekee hakiwezi kuziba pengo kubwa la ufinyu wa bajeti ya dawa na vifaa tiba muhimu ambao hauendani na mahitaji halisi. Kwa mfano, makadirio ya mahitaji ya dawa nchini kwa mwaka wa fedha 2014/15 ni shilingi bilioni 500 lakini bajeti iliyopangwa na kupitishwa ni shilingi bilioni 70.5 ambayo inakidhi mahitaji kwa asilimia 14 tu!

Sikika inapenda kuikumbusha Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii kuwa, takribani asilimia 75 ya wagonjwa  wanaopata huduma katika hospitali za Manispaa wapo katika kundi la msamaha wa huduma za afya. Kundi hili linahusisha wajawazito, watoto chini ya miaka mitano, wazee, watu wenye magonjwa sugu, watu wasiojiweza pamoja na watu wenye ulemavu. Hii inamaanisha kuwa Serikali inategemea asilimia 25 tu ya wagonjwa wanaoweza kuchangia huduma  kama chanzo  kikuu cha fedha za dawa zitokanazo na uchangiaji. Serikali inatakiwa kuwajibika katika hili na sio kuwatupia mzigo wananchi wachache.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii atambue kuwa, kuzitaka hospitali kulipa deni la MSD kwa kutumia fedha za uchangiaji badala ya kutumia fedha hizo kununua dawa kutokana na ufinyu wa bajeti, ni chanzo cha kuzifanya hospitali hizo kuendelea  kukopa zaidi na hivyo kuendelea kukuza tatizo badala ya kutafuta suluhu. Tunamkumbusha kwamba hili ni tatizo linalotokana mfululizo wa upangaji wa bajeti finyu kwa makusudi. Baadhi ya hospitali hizi zimekuwa zikitumia fedha za uchangiaji kununua dawa lakini bado zina madeni. Kwa hiyo, agizo la Waziri halitakuwa na tija katika kutatua tatizo hili kwa sasa.

Hii sio mara ya kwanza kwa Wizara ya Afya kuzitaka hospitali kupeleka MSD asilimia 50 ya mapato yao uchangiaji. Agizo hili limekuwa likijirudia tangu mwaka 2012 bila ya kuwa na usimamizi katika utekelezaji na ufuatiliaji. Kwa mfano, mwezi Julai 2014, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii aliziagiza hospitali zote kupeleka MSD asilimia 50 ya mapato yao. Kwa kuwa agizo hili limekuwa likishindwa kutatua tatizo la upatikanaji wa dawa, tulitarajia mbinu mbadala kutoka serikalini.

Sikika ingependa pia kujua ni jinsi gani hospitali ya Taifa, za rufaa na maalumu ambazo zinachangia asilimia kubwa ya deni (67%) katika kundi la madeni ya vituo vya huduma za afya zitalipa deni hilo, kwani agizo la waziri lililenga hospitali za wilaya na mikoa pekee. Vile vile, tungependa kujua Wizara imeweka mipango gani katika kulipa deni lake ambalo ni zaidi ya asilimia 70 ya deni lote ambalo MSD wanadai. Deni hilo la Wizara linatokana na gharama za kugomboa, kuhifadhi na kusambaza bidhaa za miradi misonge (vertical programs).

Mbali na hilo, tamko la Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa Umma la tarehe 27 Oktoba 2014 linaeleza kuwa, Serikali imekuwa ikilipa Deni la MSD kwa awamu. Hata hivyo, Waziri hakuweka wazi kwamba pamoja na kulipa kwa awamu, deni limekuwa likiongezeka kwa sababu serikali inalipa kiwango kidogo na kukopa kiwango kikubwa. Kwa mfano, mwaka 2013 deni lilikuwa kiasi cha Tsh. bilioni 76.4 lakini kufikia Septemba 2014 deni limekuwa na kufikia kiasi cha Tsh. bilioni 102 ingawa serikali ilifanya malipo ya Tsh. bilioni 10 .

Sikika ingependa kupata ufafanuzi kutoka kwa Waziri wa Afya na Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha, Mh. Mwigulu Nchemba ambaye hivi karibuni alinukuliwa na baadhi ya magazeti akisema kuwa kiasi cha fedha zilizotolewa kwa ajili ya dawa katika mwaka 2013/14 ilikuwa Tsh. bilioni 47 lakini ni Tsh. bilioni 7 tu ndizo zilitumika katika kununua dawa. Sikika, pamoja na watanzania wote, ingependa kujua ni wapi  fedha hizi zimepelekwa na ni kwa sababu zipi  hususan katika kipindi hiki cha uhaba wa dawa na vifaa  tiba katika vituo vya huduma za afya.

Sikika pia ingependa kutoa ufafanuzi kwa umma kwamba misaada iliyositishwa na wafadhili ni kwenye bajeti ya kuu tu (General Budget support) na si kwenye mfuko wa pamoja wa sekta ya afya (Health Basket Fund). Kwa kipindi cha Julai-Septemba 2014, zaidi ya Tsh bilioni 20 zilitolewa na wafadhili kwa ajili ya kusaidia halmashauri zote nchini ambapo kwa kawaida, theluthi moja ya fedha hizo inapaswa kutumika kwa ajili ya manununzi ya dawa na vifaa tiba muhimu.

Sikika inatambua juhudi za serikali kujumuisha sekta ya afya katika mpango wa matokeo makubwa sasa (BRN), ambao kwa kiasi unaweza kuchangia kupunguza uhaba  sugu wa  dawa na vifaa tiba katika vituo vya huduma za afya vya umma. Hata hivyo, mpango huo utaanza kutekelezwa rasmi mwaka wa fedha 2015/16, hivyo hauwezi kutatua tatizo la sasa la dawa. Waziri atambue kwamba wagonjwa wanateseka na pengine baadhi kufariki kwa sababu ya ukosefu huu wa dawa na vifaa tiba.

Mwisho, Sikika inaitaka Wizara ya afya na Ustawi wa Jamii kuchukua hatua za haraka katika kutatua tatizo hili sugu la ukosefu wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya huduma za afya vya umma. Uhaba wa dawa unawanyima wananchi kupata haki ya huduma bora za afya ambazo huweza kusababisha vifo. Serikali inapaswa kulipa deni la MSD na kuwezesha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwa dharura na haraka. Sio haki kwa serikali yoyote kuacha wananchi wake wakiteseka ama kupoteza maisha kutokanana sababu zinazoweza kuzuilika.

Mr. Irenei Kiria,

Executive Director of Sikika,
P. O. Box 12183 Dar es Salaam,

Taarifa kuhusu tetesi za uteuzi wa Konseli wa Heshima Uchina

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA 

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

Hivi karibuni kumezuka taarifa za upotoshwaji zilizotolewa kwenye mitandao ya kijamii kwamba Serikali ya Tanzania imemteua Bw. Salaah, Mkurugenzi wa Home Shopping Centre, (pichani ) kuwa Konseli wa Heshima (Honorary Consul) kwenye mji wa Guangzhou kwenye Jimbo la Guandong. 

Watoa taarifa hizo, hawakutoa ushahidi wowote kuthibitisha madai yao zaidi ya kutoa picha mbalimbali za Bw.Salaah kutoka kwenye mitandao mingine ya kijamii.

Taarifa hizo sio za kweli. 

Kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za mahusiano ya kidiplomasia ya China, nafasi ya Konseli wa Heshima haitambuliki 'mainland' China. Kwa maneno mengine hakuna nchi yoyote duniani inayoweza kuteua mtu kuwa Konseli wa Heshima katika eneo lolote la China isipokuwa Hong Kong ambako kuna mamlaka huru za utawala zinazofuata sheria zake.

Kwa faida ya umma, ni vema kufafanua kwamba Nchi ya China inakubali nchi za Nje kufungua Ubalozi kamili (Embassy) ambao makao yake yanatakiwa kuwepo katika mji Mkuu wa China- Beijing na Konseli Kuu ama kwa lugha iliyozoeleka Ubalozi Mdogo (General Consulate) ambao unaweza kufunguliwa kwenye makao Makuu ya mji wowote ule katika Majimbo ya China.

Watu wengi wamekuwa wakichanganya Ubalozi Mdogo au Konseli Kuu (General Consulate) na Konseli (Ubalozi) wa Heshima (Honorary Consulate). Konseli Kuu (General Consulate) ni sehemu ya Ubalozi (ndio maana wengi huuita Ubalozi Mdogo) ambapo kiongozi wake na maafisa wake wote ni watumishi wa Serikali kutokea Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Masharti ya kuwa Mkuu wa Konseli 'General Consulate' lazima uwe Afisa Mwandamizi wa Mambo ya Nje mwenye uzoefu usiopungua miaka 10 ya Utumishi katika Wizara ya Mambo ya Nje.

Kwa muktadha huo, taarifa kwamba Bw.Salaah ameteuliwa kuwa Balozi wa Heshima wa Tanzania huko Guangzhou sio kweli kwasababu Sheria za China haziruhusu uwepo wa nafasi hiyo. Aidha, Bw Salaah hawezi kuwa Balozi Mdogo (Consul General) kwa kuwa yeye sio mwajiriwa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Hivyo habari zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii sio za kweli na zinalenga kuupotosha umma.

IMETOLEWA NA
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

OCTOBER 30, 2014

Garden Avenue sasa ni Hamburg Avenue


Mtaa wa Garden ulioko jijini Dar es Salaam umebadilishwa jina na kuwa Hamburg Avenue.

Hafla ya kubadili jina hilo ilifanyika jijini Dar es Salaam, ambapo Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk Didas Masaburi, amesema uamuzi wa kubadili jina la mtaa huo limetokana na ushirikiano wa muda mrefu uliopo kati ya jiji la Dar es Salaam nchini Tanzania na jiji la Hamburg la nchini Ujerumani . 

Kutokana na ushirikiano katika majiji hayo katika nyanja mbalimbali ikiwemo kikosi cha zimamoto, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Philip Mwakyusa amesema Serikali ya Ujerumani itasaidia katika ujenzi wa mtambo wa kutengeneza mbolea kwa kutumia taka ngumu.

PAC yaahidi kuwalinda maafisa wa ofisi ya CAG waliotishiwa maisha na viongozi

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (Public Accounts Committee - PAC) imesema itawalinda na kuwatetea maafisa wa ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (Controller and Auditor General - CAG).

Uamuzi huo unatokana na taarifa za maafisa hao kutishiwa maisha na baadhi ya Viongozi wanaotuhumiwa kuhusika na matumizi mabaya ya fedha za umma, zaidi ya shilingi bilioni 40.

Hatua hiyo ilielezwa katika mkutano uliofanyika mkoani Mwanza, wa majumuisho ya ziara ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali ambayo iliwataka viongozi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuhudhuria mkutano huo ili kutoa majibu ya tuhuma hizo. Hata hivyo viongozi hao walipuuza agizo la kamati, hivyo kumlazimu Mwenyekiti kuuvunja mkutano huo.

Mjumbe wa kamati hiyo, Kange Lugora alisema kamati hiyo iliishauri wizara husika kushirikiana nao pamoja tangu mwanzo wa ziara yao katika majumuisho ya kamati hiyo ili kubaini yanayotendeka katika miradi ya maendeleo.

“Kitendo cha wizara kutoshiriki katika majumuisho ya kamati hii ni kuendelea kuhalalisha ubadhirifu unaoendelea kwenye halmashauri, tunaonyeshwa miradi hewa na serikali ngazi ya wizara ilipaswa wajionee wenyewe,” alisema.

Rejea: Taarifa ya CAG ya ukaguzi maalum wa IPTL wa akaunti ya Tegeta Escrow

TAARIFA KWA UMMA NA VYOMBO VYA HABARI

TAARIFA YA UKAGUZI MAALUM WA AKAUNTI YA TEGETA ESCROW
(UKAGUZI WA IPTL)


Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali inapenda kuujulisha Umma kuwa Ukaguzi Maalum wa akaunti ya Tegeta Escrow ambao unafahamika kama Ukaguzi wa IPTL unaendelea na unaongozwa na Hadidu za Rejea (ToR) zilizotolewa na kisha kuridhiwa na Ofisi ya 

Bunge na Wizara ya Nishati na Madini.

Ukaguzi wa akaunti ya Tegeta Escrow uliombwa na Katibu wa Bunge na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini. Ukaguzi huu unalenga kufanya uchunguzi wa kina ambao utatoa taarifa kamili yenye kuonesha hali halisi kuhusu miamala (transactions) kwenye akaunti maalum ya Tegeta Escrow kisha kutoa taarifa kuhusiana na ukaguzi huo.

Kwa kuwa Hadidu za Rejea pekee haziwezi kuonesha ukubwa wa kazi bali utekelezaji wa kazi yenyewe ndio unaoweza kutoa taswira halisi, ni  vyema umma wa watanzania ukatambua kuwa 
Ukaguzi huu haujaweza kukamilika kwa kipindi kilichokadiriwa awali hivyo ukaguzi unaendelea kwa kuzingatia Hadidu za Rejea na kifungu cha 29 cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma Na. 11 ya mwaka 2008.

Aidha, ongezeko la muda wa kukamilisha ukaguzi huu limetokana na uhitaji wa kukusanya maelezo yanayoendana na vielelezo vinavyojitosheleza ili kumsaidia mkaguzi kufikia malengo ya ukaguzi huo.

Ukusanyaji wa taarifa hizo unategemea wahusika kutoka Taasisi za Serikali, Mashirika ya Umma na taasisi na Watu binafsi waliopo nchini na nje ya nchi ambao ni wadau katika suala hili.

Hata hivyo licha ya changamoto zilizoainishwa hapo juu, ukaguzi wa IPTL unaendelea na muelekeo ni mzuri kwa sababu ni maeneo machache tu yaliyobakia ambapo yatakapo kamilika tutawasilisha ripoti kwa taasisi zilizouomba ukaguzi huu kwa mujibu wa Sheria.

Aidha, tunaendelea kupata ushirikiano mzuri kutoka kwa wadau wa ukaguzi huo. Ifahamike kuwa ukaguzi bado unaendelea hivyo itakuwa ni kinyume na utaratibu kwa Ofisi hii kuzungumzia kwa kina taarifa ya ukaguzi wa IPTL kwa sasa.

Ofisi hii itaendelea kutekeleza majukumu yake yote kwa kuzingatia misingi ya uwazi na uwajibikaji usiokiuka taratibu za kisheria katika kukusanya na kutumia rasilimali za umma.

Imetolewa,
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano
Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi

Thursday 30 October 2014

HII NI KWA WANAWAKE NA WASICHANA WANAOPITIA CHANGAMOTO MBALI MBALI ZA KIMAISHA.


umekuwepo na hali ya kuchaguliana nini cha kufanya kwenye maisha.Hali ambayo hupelekea wengine kupata msongo wa mawazo kisa kuona hawakubaliki katika jamii fulani.Au kuona kuwa hathaminiki kisa ana utaratibu flani wa kimaisha tofauti na wengine.

Kumcheka mtu kwa sababu ya muonekano fulani bila kujali kuwa huo muonekano umekuja baada ya kupitia changamoto fulani katika maisha.Wakati mwingine wanawake ndio hao hao hukaa na kunyoosha vidole kumcheka mwanamke mwenzao.Wasichana wanamkejeli na kumdhihaki msichana mwenzao kisa muonekao or style flani ya maisha.Nimetumia mfano wa wanawake kwa sababu ndio wanaongoza kwa tabia hiyo dhidi ya wanawake wenzao.



Picha hizi ni kazi ya mwanadada Carol Rosseti wa Brazil.Amechora na kutengeneza picha hizi kuwatia moyo na kuiasa jamii kuacha maneno ya dharau na kejeli kwa wanawake.

 


b







Je wewe upo wapi?

MAISHA NI MAPAMBANO,KILA SIKU NI MAPAMBANO.

Kila siku za maisha yetu tunapitia mapambano mbali mbali na changamoto mbali mbali.
Likiisha hili unahisi utakaa kwa raha lakini baadae litakuja lingine.Changamoto kwenye kazi kawaida huwa tunaita matatizo mie natumia neno changamoto.Kama sio kwenye kazi basi kwenye,biashara,nyumbani,kwenye mahusiano yako,kwa majirani,marafiki,watoto,pesa,jamiii yaani likiisha hili baada ya muda linakuja hili.

Usitarajie utakaa kwa starehe mwenyewe ndio maana kila jambo lina kinyume chake.Raha karaha,tabasamu kinyume chake huzuni,kicheko kinyume chake kilio n.k

Napenda ni kwambie vyovyote iwavyo lazima maisha yaendelee.Maisha hayatakiwi kusimama.Tatizo linapojitokeza usipaparike ukatapatapa TULIA.Tuliza akili tafakari na uweze kuona vyema namna utakavyojitoa kwenye tatizo husika.Ukipaparika utashindwa kuona vyema na badala ya kutatua tatizo ukaongeza tatizo.

Pia kubwa angalia CHANZO cha tatizo husika ni nini ili usolve ukijua unasolve nini?tatizo la aina gani
Kwa sababu ya wahaka na roho kuwa juu na maumivu ya tatizo husika unakuta unakuwa na huzuni,hasira,uchungu, ambao unaweza kuzidisha na kuzalisha tatizo jipya hata ukija kutaka kutatua tatizo chanzo hukioni kwa sababu tayari umejijazia matatizo.

Hakuna hali ya kudumu kuwa na imani,kuwa mvumilivu na mwenye subira.Usikae chini ukasema yaani jamani kila siku mimi tu mimi tu matatizo yananiandama kila mtu ana mapambano yake na anapambana nayo kivyake.Usikae chini ukajihurumia simama.

Wakati mwingine matatizo na changamoto ukiyatazama vizuri yanaweza kuwa fursa.Sio yote inategemea ni tatizo gani.

Litambue tatizo,usipaparike stay calm,acha mawazo na akili yako yawe chanya ili uweze kuona vyema na kutafakari vyema.Kuwa kwenye control sio tatizo ndio likucontrol wewe.

*Haya ni mawazo yangu kama mdau unaweza kujazilizia mtazamo wako pindi tunapopitia changamoto mbali mbali za kimaisha tufanyeje?*

*wewe hufanyaje nyakazi za matatizo na changamoto?*

*Hapo siongelei Msiba au kifo.

Na Dina Marios.

NI WAJIBU WAKO KAMA MZAZI KUMJENGEA MTOTO WAKO KUJIAMINI.

Huwa nasoma sana website inaitwa woman of christ nilikutana na huu ujumbe nikapenda kushare nanyi.Hasa wazazi itawafaa katika malezi.

Mzazi ni wajibu wako kuwapenda watoto wako wote, kuwafundisha njia ipasayo, kuwatia moyo wanapopitia magumu, na kuhakikisha unakuwa mstari wa mbele kuwajengea self esteem imara. Mzazi hupaswi kuwa critic wa mtoto wako, hiyo sio kazi yako. Muongoze katika kweli, mfundishe, muadhibu pale anapokosea na chunga sana usimuadhibu ili kumuaibisha bali kumsaidia. Adhabu ya kumsaidia mtoto unampa kwa kujali utu wake na sio mbele ya kadamnasi na kumuaibisha.
Watoto hawalingani, usifanye kosa la kuwalinganisha watoto, iwe ni watoto wako wote au kumlinganisha wako na wa jirani. Tambua kila mwanadamu ameumbwa tofauti, jitahidi kumfahamu mwanao na kumsaidia kuwa bora kwa jinsi Mungu alivyomuumba ukiangalia zaidi strengths zake kuliko mapungufu. Kosa ambalo wazazi wengi wanafanya ni kuwabagua watoto kulingana na uwezo wao kwa yale ambayo yanaonekana mema katika jamii mfano kumpenda zaidi mtoto anayejituma kuwahi kuamka na kumbeza yule anayependa kulala tena mbele za wengine. Ndio, kila mtoto lazima afuate utaratibu lakini usitumie kigezo hiki kupimia upendo, badala ya kumsaidia utakuwa unampoteza kabisa.

Mtoto anayeona anabaguliwa nyumbani atajenga kiburi na ataanza kuwachukia wenzie wanaopendwa zaidi na itampelekea kutafuta upendo nje kwa watu wasiofaa na kujikuta katika matatizo makubwa. Chunga sana maneno unayomwambia mtoto wako, maneno yanaumiza kwa muda mrefu, yanaua kujiamini na yanaumba. Mtamkie maneno ya baraka, tumaini na hata pale unapomuonya maneno yako yasiwe ya kumdhalilisha mfano hujui kitu kabisa, sijui wewe ni mtoto wa aina gani, hufai kabisa n.k. Maneno ya aina hiyo hayafai kabisa maana hayajengi bali yanamuondolea kujiamini na kumfanya ajione hana thamani

Shule yampiga marufuku mwanafunzi kuhudhuria masomo kwa hofu ya Ebola

School bans girl amid Ebola fear; family suesStori kuhusiana na watu wanaotengwa kwa kuhisiwa kuwa wana maambukizi ya Ebola bado zimeendelea kusikika kutoka sehemu mbali mbali duniani, ambapo kwa sasa mzazi mmoja ameifungulia mashtaka shule kutokana na shule hiyo kumzuia mtoto wake wa kike asihudhurie masomo shuleni hapo mpaka zitakapopita siku 21.
Baba wa mtoto huyo ameitaka mahakama kutoa amri kwa shule iliyopo Milford, Connecticut Marekani kumruhusu mtoto wake aendelee na masomo kwa kuwa hakuonesha dalili zozote za kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo.
Shule hiyo haikutoa jibu lolote kuhusiana na maombi ya mzazi huyo, kitu kilichompelekea kufungua mashtaka katika mahakama ya wilaya ya Connecticut.
Mtoto huyo amekumbana na kadhia hiyo baada ya kusafiri kwenda na kurudi Lagos, Nigeria akiwa na baba yake kati ya tarehe 2 na 13 Oktoba, ndipo shule hiyo ilimzuia mwanafunzi huyo kuhudhuri masomo shuleni mpaka tarehe 3 mwezi Novemba na badala yake shule itakuwa ikimtumia mwalimu kwa ajili ya kumfundisha akiwa nyumbani kwao.
Tangu kulipuka kwa Ebola katika nchi za Afrika Magharibi, kumekuwa na mfululizo wa matukio ya kutengwa kwa watu wanaotokea Afrika Magharibi nchini Marekani ambapo chuo kimoja Texas kilisitisha kupokea maombi ya kujiunga na masomo kwa watu kutoka Nigeria kwa hofu ya maambukizi ya virusi vya ugonjwa huo.

HAYA NDIO MAUMIVU YA AJALI YA ARUSHA

Simanzi zimetanda jiji la Arusha baada ya watu zaidi ya 15 kufa katika ajali iliyotokea eneo la Tengeru. Akiongea na mwandishi wetu mmoja ya mashahidi aliyefika eneo la tukio na hospitali ya Mount Meru amesema ajali ilitokea majira ya saa kumi jioni huko maeneo ya Sadec-Darajani -Tengeru iliyohusisha gari la abiria aina ya Hiace linalobeba watu toka Usa-River kwenda Arusha mjini na Lori la mafuta.Aliongeza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva wa hiace (gari la abiria) iliyokuwa ikijaribu kupita magari mengine ndiyo akakutana uso kwa uso na lori hilo. Habari kamili zitawajia punde. 










PINDA AENDELEA NA ZIARA OMAN

1Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mkurugenzi Mtenda wa Shirika la Maendeleo ya Petroli la Oman (PDO), Bw. Raoul Resticci baada ya kuwasili kwenye makao makuu ya Shirika hilo ili kujifunza shughuli za uwekezaji na uvunaji wa gesi na mafuta . Alikuwa katika ziara ya kikazi nchi OmanOktoba 28, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 2Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Naibu Waziri Mkuu wa Oman, Mhe. Sayyi Fahad Al Said   (kushoto kwake) wakizungumza na balozi wa Tanzania nchini Oman, Ali Ahmed Saleh katika dhifa aliyoandaliwa Waziri Mkuu kwenye hoteli ya Al Bustan mjini Muscut Oktoba 28, 2014. Wapili kulia ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Dr. Titus kamani na watatu kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maalim Mahadhi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)3Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akisalimiana na baadhi ya mabalozi wanaowakilisha wa nchi mbalimbali  nchini   Oman katika dhifa aliyoandaliwa na Naibu Waziri Mkuu wa Oman, Mhe. Sayyid Fahad Al Said (kulia) kwenye hoteli ya Al Bustan  mjini Muscut Oktoba 29, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)5Waziri Mkuu, MIzengo Pinda akizungumza na Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Uhusiano wa Serikali ya Oman , Ahmed Bin Salim Al Harthy baada ya kutembelea  Msikiti wa Sultan Qaboos Grand uliopo Muscut ambao ni moja kati ya misiki mikubwa na yenye kuvutia sana dunianiOktoba 29, 2014. Kulia ni balozi wa Tanzania nchini Oman, Ali Ahmed Saleh.Yuko katika ziara ya kikazi nchini Oman. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 7Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiweka saini kitabu cha wageni baada ya kutembelea msikiti wa Sultan Qamboos Grand uliopo Muscut ambao ni kati ya misikiti mikubwa na inayovutia duniani Octoba 29, 2014. Kushoto ni Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa serikali ya Oman, Ahmed Bin Salim Al Harthy. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 8Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akipokea kutoka kwa Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa serikali ya Oman, Ahmed Bin Salim Ali Harthy zawadi ya kitabu kinachoonyesha Msikiti wa Sultan Qamboos Grand uliopo Muscut baada ya kuutembelea msikiti huo akiwa katika ziara ya kikazi nchini Oman, Oktoba 29, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)9Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda  akipokea  kutoka kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Uhusiano wa Serikali ya Oman, Ahmed Bin Salim Al Harthy zawadi  ya kitabu baada ya kutembelea msikiti wa Sultan Qamboos Grand wa Muscut ambao ni kati ya misikiti mikubwa na yenye kuvutia duniani. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 10Moja ya barabara za jiji la Muscu, Oman.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)11Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na baadhi ya wafanyabiashara wa Oman kwenye hoteli ya Al Bustan mjini Muscut, Oktoba 29, 2014. (Pichsa na Ofisi ya Waziri Mkuu) 12Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyabiashara wa Oman baada ya kuzungumza nao kwenye hoteli ya Al Bustan mjini Muscut Oktoba 29, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 13Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na mmoja wa wafanyabiara wa Oman wanaokusudia kuwekeza Tanzania, Sheikh Abdullah Al- Zakwani baada ya kikao chake na wafanyabiashara wa Oman kwenye hoteli ya Al Bustan, Muscut Oktoba 29, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

RAIS MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE AKIWASILI NCHINI LEO.

unnamed
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange (kushoto) leo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere pamoja na baadhi ya viongozi wengine mara baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi nchini China na Vietnam.

Mbowe: Ukawa sasa ni mbele kwa mbele


Muungano wa Ukawa dhidi ya CCM, ni matokeo ya misuguano iliyojiri wakati wa mchakato wa Katiba. Hatua ya kwanza ilianza kwa Mbowe kuunda Baraza la Mawaziri Kivuli, likiwashirikisha wabunge kutoka vyama hivyo isipokuwa NLD ambacho hakina mwakilishi bungeni.
Wakosoaji
Mbunge wa Mbinga Magharibi (CCM), Kapteni John Komba alisema ushirikiano huo ni feki na unalenga katika masilahi binafsi na kwamba hauwezi kukiyumbisha chama chake. Pia alisema kukosekana kwa wanawake wa kutosha kwenye mkutano huo wa juzi ni dalili tosha ya anguko la Ukawa.
“Ukiona wapinzani wanaungana ujue wamegundua nguvu ya kila mmoja wao haitoshi kuing’oa CCM, lakini swali la msingi kujiuliza ni je, muungano huo utaleta tija inayokusudiwa? Watasambaratika baada ya muda mfupi na masilahi binafsi pamoja na itikadi tofauti ndizo zitakazochangia,” alisema Komba.
Komba alisema aliangalia mkutano huo kupitia runinga lakini alishangazwa na idadi ndogo ya wanawake waliohudhuria na kusema kuwa hiyo ni ishara kuwa kinamama hawaukubali umoja huo.
Mwenyekiti wa APPT-Maendeleo, Peter Mziray alisema: “Hili si jambo jipya kwa kuwa lilishawahi kutokea lakini baada ya kuona halina maana wengine tuliamua kujitoa… tumekaa pembeni tuone watakapofika.
“Huko mbele ni lazima watakorofishana hasa litakapokuja suala la masilahi. Inaeleweka wazi kuwa chama chenye wawakilishi wengi ndicho kinapata ruzuku. Kusimamisha mgombea wa urais pekee ina maana kubwa kwa kila chama, sijui kama wameweka wazi utaratibu wa kugawana ruzuku itakayopatikana kwa chama kitakachostahili.”
Mziray alibainisha kuwa anakumbuka vizuri ushirikiano uliokuwapo kati ya Chadema na Mchungaji Christopher Mtikila ambaye baada ya kukiunga mkono chama hicho hakuambulia chochote.
Kwa upande wake, Mtikila ambaye ni Mwenyekiti wa DP aliuponda muungano huo akisema: “Nililetewa mwaliko wa kuhudhuria mkutano uliofanyika juzi kutoka kwa mratibu wa Ukawa, ambaye simjui. Siwezi kwenda huko kwa sababu wakati wanaanzisha Ukawa ilikuwa ni Umoja wa Katiba ya Watanganyika na si kama wanavyoieleza.”
Alidai kwamba ndiye aliyeanzisha mchakato wa kudai Katiba ya Watanganyika baada ya Rais Jakaya Kikwete kulihutubia Bunge Maalumu la Katiba lakini baada ya Chadema kuchukua hatamu za kuongoza harakati hizo alijiweka pembeni.
Wabunge wa upinzani
Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Peter Msigwa alisema nafasi za uongozi katika ushirikiano wa Ukawa zipo wazi kwa kila mwanachama, hivyo ushindani utahusisha wote walio tayari kushindana.
“Jimbo si mali ya mbunge aliyepo, kitakachoendelea kumweka madarakani ni uchapakazi wake licha ya kuungwa mkono na Ukawa. Yapo maeneo yanatambulika kuwa ni ngome za vyama fulani vya upinzani huko, tutaunga mkono ili kupata ushindi mkubwa zaidi. Katika maeneo ambayo CCM wanaongoza juhudi binafsi ndizo zitakazotumika kumpata mpinzani atakayeungwa mkono na wote.”
Mbunge wa Lindi Mjini (CUF), Barwan Salum alisema historia inaonyesha kuwa vyama vya upinzani vinaongoza katika maeneo tofauti na kwamba juhudi hizi zinalenga kuwanufaisha wananchi.
“Chadema ina nguvu kubwa Kaskazini mwa nchi wakati NCCR-Mageuzi ikiongoza Magharibi na CUF wanafanya vizuri Visiwani. Katika chaguzi zilizopita, takwimu zinaonyesha kuwa vyama vya upinzani kwa jumla wake vilikuwa vinapata asilimia 40 ya nafasi zote. Umoja huu unamaanisha makubwa katika siasa za nchi hii.”
Wananchi
Mkazi wa Magomeni, Dar es Salaam, Hamis Suleiman (72), alisema muungano huo ni mwamko mpya wa siasa nchini kwani hakuwahi kufikiria kuwa kuna siku wapinzani watakuja kuonyesha mshikamano mkubwa kiasi hicho katika kupigania masilahi ya taifa.
“Ni kitu kipya katika historia ya Taifa letu. Wakati tunadai uhuru iliwezekana kuona mambo haya lakini kwa sasa naona harakati hizo zinafanywa kudai utawala bora na usawa kwa wananchi wote,” alisema Suleiman.
Mkazi mwingine, Deogratius Bikongoro alisema hakuamini kama wapinzani wanaweza wakafanya kitu kikubwa kama hicho, tena hadharani na kwamba alishawishika kwenda kwenye mkutano huo ili aweze kujiridhisha.
“Nimejifunza elimu ya uraia katika tukio hili. Kumsikiliza Tundu Lissu na Ismail Jussa Ladhu wakifafanua Katiba Inayopendekezwa pamoja na sheria za nchi kwa jumla, imenipa ufahamu wa mambo mengi niliyokuwa siyajui lakini nimeona dhamira ya wapinzani sambamba na mwitikio wa wananchi. Mkutano huu unatoa picha kuwa hata huko mikoani kuna watu ambao hawajaridhika na jinsi mchakato wa Katiba ulivyokwenda,” alisema.
Mmoja wa waasisi wa Chadema, Victor Kimesela alisema mchakato wa kuunganisha vyama vya upinzani ulianza siku nyingi kutokana na mahitaji ya wananchi… “Wananchi watanufaika kutokana na muungano huu ambao unaunganisha juhudi tofauti zinazoletwa na itikadi mtambuka.”
Alisema juhudi za kuunganisha vyama zimepitia hatua nyingi na kuzitaja kuwa ni pamoja na kuundwa kwa Umoja wa Demokrasia Tanzania (Udata) na Kamati ya Mabadiliko ya Katiba (Kamaka) na kusisitiza kuwa Ukawa ndiyo hitimisho la juhudi hizo.
Mkurugenzi wa Fedha wa CUF, Joran Bashange alisema:
“Masilahi ya Taifa ndiyo kitu cha msingi kinachotuunganisha pamoja na tunawaomba wote walio tayari kushirikiana nasi watuunge mkono katika kutekeleza azma hii muhimu kwa wananchi na nchi kwa ujumla. Masilahi binafsi siyo hoja yetu kwa kuwa wapo watu wengi wasio wafuasi wa siasa hapa nchini lakini wanaovutiwa na haja ya kuwa na maendeleo sawa kulingana na rasilimali zilizopo.”
Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini wa NCCR-Mageuzi, Mohamed Tibanyendera alisema kitendo cha CCM kutunga Katiba yenye mapendekezo yake pekee na kuyatupia kisogo maoni ya wananchi, kimepokewa vibaya na Watanzania wengi ambao wanataka mabadiliko kupitia umoja huu.
Mbunge wa Gando (CUF), Khalifa Suleiman Khalifa alisema: “Historia inaonyesha kuwa ni vigumu kwa vyama vya upinzani kukiondoa madarakani chama tawala pasipo ushirikiano wa vyama hivyo. Tuliona yaliyotokea Afrika Kusini na hata jirani zetu Kenya… muungano huu utaleta mapinduzi kama yaliyotokea Kenya.”

MAHAKAMA KUU YA MAREKANI YAKATAA KUPITIA HUKUMU YA NDOA YA JINSIA MOJA


Picha ,hii imepigwa juma-mosi Oktoba,2014 ikiwaonyesha wana-ndoa wa jinsia moja wakiwa wamekaa mkao maalumu kwa ajili ya kupigwa picha (pose), mara baada ya kufunga ndoa ,Inslington London,Natalie Banner (kushoto)bwana harusi na Elyisia Rose Johnson (kulia bibi harusi),ndoa za jinsia moja kati ya mwana ume kwa mwanaume, mwanamke kwa mwanamke,zimeenea katika nchi nyingi hasa zilizoendelea baada ya kipindi kirefu ,hata hivyo hivi karibuni nchini marekani ,Mahakama moja ya juu imekataa kupitia upya hukumu iliyotolewa miaka ya nyuma ya kupiga marufuku  ndoa ya jinsia moja iliyotolewa miaka ya,bado katika baadhi ya majimbo nchini Marekani haya-ruhusu ndoa za jinsia moja.

President Kikwete has sent a congratulatory message to Her Excellency Dilma Rousseff on the occasion of her re-election as President of the Federative Republic of Brazil

Brazil-President_Mill
H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to Her Excellency Dilma Rousseff on the occasion of her re-election as President of the Federative Republic of Brazil.
The message reads as follows.
“Her Excellency Dilma Rousseff
  The President of the Federative Republic of Brazil,
  Brasilia,
  BRAZIL.
I have received with great pleasure the news of your re-election to the highest office of your country. On behalf of the Government and people of the United Republic of Tanzania and indeed on my own behalf, I wish to convey my sincere and warmest congratulations to You and through you to the Government and the people of the Federative Republic of Brazil for your election to the Presidency of Brazil.
Your re-election is a sign of the trust and confidence that the people of Brazil have in your leadership qualities. As you continue discharging the noble duties bestowed upon you, I would like to assure Your Excellency of my continued co-operation in further strengthening the bilateral relations that so happily exist between our two countries.
Please accept, Your Excellency, my personal regards and best wishes for your continued good health and success”.
ISSUED BY: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM
29TH OCTOBER, 2014

Wednesday 29 October 2014

BREAKING NEWS: RAIS WA ZAMBIA MICHAEL SATA AMEFARIKI DUNIA

Sata, 77, had been in office since September, 2011 [AP]
Zambian President Michael Sata has died in London, where he had been receiving treatment for an undisclosed illness, three private Zambian media outlets said.
 The reports on the private Muzi television station, and the Zambia Reports and Zambian Watchdog websites, said the southern African nation's cabinet was about to meet.
 Government officials gave no immediate comment.
The reports said Sata had died on Tuesday evening at London's King Edward VII hospital. The hospital declined to comment.

Sata, 77, left Zambia for medical treatment on October 19 accompanied by his wife and family members, according to a brief government statement that gave no further details.

There has been no official update on his condition and acting president Edgar Lungu had to lead celebrations last week to mark the landlocked nation's 50th anniversary of independence from Britain.
Concern over Sata's health has been mounting in the country since June, when he disappeared from the public eye without explanation and was then reported to be getting medical treatment in Israel.
He missed a scheduled speech at the UN General Assembly in September amid reports that he had fallen ill in his New York hotel.
A few days before that, he had attended the opening of parliament in Lusaka, joking: "I am not dead." Sata has not been seen in public since he returned to Zambia from New York in late September.
Sata, who once worked as a railway porter in London, had been the country's president since September, 2011 after winning a tight presidential race against the then incumbent, Rupiah Banda.


SOURCE ALJAZEERA ENGLI

Tuesday 28 October 2014

Mambo yazidi kuiva Karibu Music Festival

Px 1
WASANII kutoka ndani na nje wanatarajiwa kupamba tamasha la Muziki la Kimataifa la ‘Karibu Music Festival’ litakalofanyika kwa siku tatu kwenye mji wa Kihistoria wa Bagamoyo, Novemba 7 hadi 9 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) mapema Oktoba 27, Msemaji wa tamasha hilo Muslim Nassor ‘Jazzphaa’ alisema maandalizi yamekamilika na tayari wasanii wa awali waliopatikana wapo hadharani wanaendelea na matayarisho huku akiwaomba watanzania na wadau wa burudani kujitokeza kwa wingi kwenye tamasha hilo.
Jazzphaa aliwataka baadhi ya wasanii wa nje na ndani na nchi zao katika mabano ni Panda (Japan), Maria Kate (Ufaransa), IFE Pianki (Uganda), Masayo (Japan), Fantuzz (Marekani), Shiwe Musique (Comoro), Dwembede (Kenya) na Mbiye Ebrima (Guinea).
Kwa upande wa
viingilio, alisema kitakuwa ni sh 5,000 kwa kila Mtanzania huku kwa
atakayekata tiketi ya siku tatu, kwa pamoja, ni sh. 12,000.
“Tamasha
hili litakuwa likifanyika usiku na mchana. Wasanii wote watakaokuwepo
katika tamasha hili watalazimika kupiga muziki kwa kutumia ala za asili
za muziki ‘Live’ na siyo ‘Playback’” alisisitiza Jazzphaa.
Kwa
upande wake, Meneja wa tamasha hilo, Richard Lupia alisema tamasha
hilo mbali ya burudani, wasanii pia watapata nafasi ya kujifunza jinsi
ya kuunadi muziki wao duniani kwa njia mbali mbali ambako kutakuwa na
warsha kutoka kwa wataalamu toka pembe zote za dunia.
Pia alisema katika tamasha hilo kutakuwa na sanaa za Michoro, mavazi na kuchonga zitakuwa zikioneshwa eneo la tamasha.
“Semina
na mijadala ya jinsi ya kuupeleka muziki wa Tanzania katika hatua
nyingine za kimaendeleo zitatolewa kwa wasanii mbalimbali. Mbinu za
kuuza kazi zao kwenye masoko ya kimataifa na kutafuta soko duniano kote
hii itakuwa fursa kwa wasanii na wadau wa sanaa hapa hapa nchini”
alisema Lupia.
 Makundi na
majina ya wasanii kutoka nyumbani ni pamoja na Afrikabisa Band,
Wahapahapa, Segere Original, Jahazi, The Spirit Band na Mama Africa.
Wengine
ni Cocodo Band, Hokororo Band, Swanu Gogo Vibes, Swahili Vibes, Fimbo
Band, Abeneko Music, Man Kifimbo, Saganda na Msafiri Zawose.
Wasanii
wengine ni Msafiri Zawose ‘Chibite Zawose’, Tongwa Ensemble, Leo
Manyika, Swahili Blues, Profesa Jay, Shilole, Juma Nature, Barnaba,
Vitalis Maembe na Jhikoman.
Aidha,
Jazzphaa aliongeza kuwa lengo la tamasha hilo ni kukuza na kurasimisha
tasnia ya muziki kwa umakini zaidi na kukuza uchumi wa eneo la
Bagamoyo ambalo ni la kihistoria.
PICHANI JUU:
Msemaji wa
tamasha la Karibu Music Festival, MAuslim Nassor ‘Jazzphaa’ (katikati)
akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho
huo.

President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete last leg of official visit to Vietnam

ho6 
:President Dr Jakaya Mrisho Kikwete shown some historical items as
he visits the Garment 10 Corporation textile mill at Nguyen Van Linh
Street in Sai Dong Ward, Gia Lam District, Hanoi on  his last leg of
his two-day official visit to Vietnam today October 28, 2014
ho7 

President Dr Jakaya Mrisho Kikwete visits the Garment 10
Corporation textile mill at Nguyen Van Linh Street in Sai Dong Ward,
Gia Lam District, Hanoi on his last leg of his two-day official visit
to Vietnam today October 28, 2014
ho1 

President Dr Jakaya Mrisho Kikwete visits the Garment 10
Corporation textile mill at Nguyen Van Linh Street in Sai Dong Ward,
Gia Lam District, Hanoi on his last leg of his two-day official visit
to Vietnam today October 28, 2014
ho2 

President Dr Jakaya Mrisho Kikwete lies a wreath at
the Mausoleum of the First President Ho Chi Minh in Hanoi on  his last
leg of his two-day official visit to Vietnam today October 28, 2014
ho3 

President Dr Jakaya Mrisho Kikwete lies a wreath at
the Mausoleum of the First President Ho Chi Minh in Hanoi on  his last
leg of his two-day official visit to Vietnam today October 28, 2014
ho4 

President Dr Jakaya Mrisho Kikwete visits the Hung Fen Food Stuff
Corporation at Trung Son in Hanoi on his last leg of his two-day
official visit to Vietnam today October 28, 2014 ho5 

President Dr Jakaya Mrisho Kikwete in a souvenir photo with
workers of  the Garment 10 Corporation textile mill he visited at
Nguyen Van Linh Street in Sai Dong Ward, Gia Lam District, Hanoi on
his last leg of his two-day official visit to Vietnam today October
28, 2014

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MAONESHO YA MWEZI WA WANAWAKE WAJASILIAMALI (MOWE) JIJINI DAR ES SALAAM.

1Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Janeth Mbene, wakati aliwasili kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 28, 2014 kwa ajili ya kufungua rasmi Maonesho ya mwezi wa Wanawake Wajasiliamali (MOWE). Picha na OMR 2Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja Masoko wa Kampuni ya GS 1, Ester Budili, wakati alipokuwa akitembelea katika mabanda ya maonesho ya Wajasiliamali, wakati wa ufunguzi wa Maonesho hayo ya mwezi ya Wanawakae wajasaliamali (MOWE) yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Oktoba 28, 2014. Kulia ni Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Janeth Mbene. Picha na OMR 3Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi msaidizi wa Kampuni ya Kazymate, Mariam Mjewa, kuhusu Jarida maalum la ‘Mchakarikaji’  wakati alipokuwa akitembelea katika mabanda ya maonesho ya Wajasiliamali, wakati wa ufunguzi wa Maonesho hayo ya mwezi ya Wanawakae wajasaliamali (MOWE) yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Oktoba 28, 2014. Picha na OMR 4Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea katika mabanda ya maonesho ya Wajasiliamali, wakati wa ufunguzi wa Maonesho hayo ya mwezi ya Wanawakae wajasaliamali (MOWE) yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Oktoba 28, 2014. Picha na OMR 5Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia Chupa ya kinywaji cha Dodoma Wine wakati alipokuwa akitembelea katika mabanda ya maonesho ya Wajasiliamali, wakati wa ufunguzi wa Maonesho hayo ya mwezi ya Wanawakae wajasaliamali (MOWE) yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Oktoba 28, 2014. Picha na OMR 6 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia Viatu (makubazi) na kusikiliza maelezo kutoka kwa Bi Hadija Rashid wa Kikundi cha Wajasiliamali cha Vumilia Corporation kutoka Pemba, wakati alipokuwa akitembelea katika mabanda ya maonesho ya Wajasiliamali, wakati wa ufunguzi wa Maonesho hayo ya mwezi ya Wanawakae wajasaliamali (MOWE) yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Oktoba 28, 2014. Picha na OMR 7 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia bidhaa na kusikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kikundi cha Wajasiliamali Walemavu cha Women Clief Mafinga, Fatina Kangessa, wakati alipokuwa akitembelea katika mabanda ya maonesho ya Wajasiliamali, wakati wa ufunguzi wa Maonesho hayo ya mwezi ya Wanawakae wajasaliamali (MOWE) yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Oktoba 28, 2014. Picha na OMR 8Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mratibu wa Kitaifa wa Program kuendeleza Ujasiliamali kwa Wanawake, Noreen Toroka, wakati alipokuwa akitembelea katika mabanda ya maonesho ya Wajasiliamali, wakati wa ufunguzi wa Maonesho hayo ya mwezi ya Wanawakae wajasaliamali (MOWE) yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Oktoba 28, 2014. Picha na OMR
9Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya ufunguzi rasmi wa Maonesho ya mwezi ya Wanawakae wajasaliamali (MOWE) yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Oktoba 28, 2014. Picha na OMR
10Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa vikundi mbalimbali na wageni waalikwa katika maonesho hayo. Picha na OMR 11Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa vikundi mbalimbali na wageni waalikwa katika maonesho hayo. Picha na OMR