TAFUTA CHOCHOTE NDANI YA NKEMA

Thursday 23 January 2014

JINSI YA KUFUGA KUKU WA KIENYEJI KWA NJIA BORA ZAIDI

Idadi ya wanyama wanaofugwa kwa chakula imezidi ile ya binadamu zaidi ya mara mbili kote ulimwenguni. Kuna maelfu ya wanyama kote duniani ilihali ni wachache tu wanaoweza kufugwa. Kati ya hawa wanyama, ni aina nne (Ng'ombe, kondoo, mbuzi na kuku) wanaochukua asilimia 95% ya wanyama wote wanaofugwa. Wanyama hawa hupatikana katika nchi za hari kwenye nyanda za chini. Lakini kati ya mifugo hawa, kuku ni maarufu katika nchi za hari na hata kote ulimwenguni.

NAMNA YA KUANZISHA BIASHARA

  Ukitaka kufanya biashara yoyote ile unatakiwa kufanya utafiti. Kutokufanya utafiti ni chanzo cha biashara nyingi kuharibika. Lazima ujiulize kwamba unataka kufanya biashara gani? Usiseme unataka kufanya biashara yoyote ile kwani kusema kwamba unataka kufanya biashara yoyote ile ni kupoteza mwelekeo kwa kuwa utakuwa hujui unataka kufanya nini. Kama hujui cha kufanya hakuna kitu utakachokifanya. Hili ni tatizo la watu wengi. Hata baadhi ya watu niliokutana nao wakitaka ushauri wamekuwa wakisumbuliwa na tatizo hili. Njia ya kukusaidia kuamua ufanye biashara gani ni kwa kujiuliza umewahi kufanya kazi au biashara gani? Umesomea nini? Vipaji vyako ni vipi? Ni biashara ipi au kazi ipi unapenda zaidi kuliko nyingine na kwa sababu gani? Ukisha jiuliza maswali haya chukua kalamu na karatasi uandike maswali yako na kuyajibu. Ukikagua maswali na majibu yako utagundua shughuli unayoipenda, unayoiweza na una kipaji nayo na hiyo ndiyo inayokufaa. Ukishachagua biashara unayoipenda ni rahisi sana kufanikiwa kwani shughuli utazifanya kwa hiyari bila kujilazimisha. Kama unashindwa kuamua ni biashara gani ufanye, soma sura ya sita katika kitabu hiki. Nimeelezea kuhusu mawazo yanayoweza kukusaidia kuanzisha biashara mbalimbali ambazo unaweza kuzifanya. Kama utakuwa bado hujafikia uamuzi baada ya hapo basi tafuta na wasiliana na washauri ili mbadilishane mawazo na ufundishwe jinsi ya kuamua ufanye biashara gani.
Mambo mengine unayotakiwa kuyafanyia utafiti ni:-

Sunday 5 January 2014

WANAWAKE WA SHOKA ULIMWENGUNI AKIWEMO MAMA GETRUDE MONGELA. SOMA HISTORIA YAKE FUPI

Kama kuna wanawake wa kitanzania ambao wameweza kuionyesha dunia kwamba Tanzania nayo ina wanawake wa shoka, basi Mama Gertrude Mongella naye yumo tena katika namba ya juu, hakosi katika namba tatu bora za mwanzo...nani anabisha? Mama huyu ambaye ni mwanasiasa, mwalimu, mwanaharakati, mke na mama wa watoto wanne, ndiye yule aliyeuongoza mkutano wa nne wa dunia kuhusu wanawake uliofanyika Beijing China mwaka 1995. Na ni huyu huyu ambaye ni rais wa kwanza wa bunge la afrika lililoundwa mwaka 2004. Ndugu wasomaji wangu naomba mjue kwamba bunge hili si la kina mama peke yake, ni bunge mchanganyiko. Kwahiyo mwanamama huyu kitendo cha kuwabwaga wanaume wote wa Afrika tena katika uchaguzi wa mara ya kwanza si kitu masihara kabisa.

Kabla sijaendelea zaidi kuwapasha juu ya mambo ambayo mama huyu ameshawahi kuyafanya, ningependa niwadokeze kidogo juu ya maisha yake binafsi.

Mama Gertrude Mongella alizaliwa katika kisiwa cha Ukerewe, mkoani Mwanza mwaka 1945 akiwa ni mmoja kati ya watoto wanne katika familia yao. Baba yake Patrice Magologozi alikuwa ni mjenzi, fundi seremala na mwanaharakati akikabiliana na siasa za mkoloni. Mama yake Bibi Nambona alikuwa ni mkulima stadi. Alizaliwa kipindi ambacho ubaguzi kati ya watoto wa kike na wakiume katika jamii yao ulikuwa umeshika hatamu, wanawake walizuiliwa mambo mengi, mfano kuongea mbele ya wanaume, kula vyakula baadhi ya vyakula au sehemu zilizonona za nyama, mfano mapaja ya kuku,firigisi mayai na vinginevyo vingi. Gertrude aliliona hili na rohoni mwake hakukubaliana nalo kabisa, lakini anamshukuru sana baba yake ambaye alikuwa akimtia moyo na kumwambia asifungwe na hizo mila na desturi ale anachotaka, aseme anapoona pana ukweli na shule atakwenda.

Alipokuwa na umri wa miaka 12, alianza shule iliyokuwa ikiendeshwa na watawa wa Maryknoll Nuns, Shule hii ilikuwa na malengo ya kuwaelimisha na kuwanyanyua watoto wa kike. Na hii ndio ilikuwa mara yake ya kwanza kusafiri toka azaliwe.

Baadaye alijiunga na chuo kikuu cha Dar es Salaam ambako alipata Shahada ya elimu. Mwaka 1975 aliingia katika siasa na kuwa mwanachama katika Baraza la kutunga sheria la Afrika Mashariki (EALA).

Tangu wakati huo, amekuwa akishikilia nafasi nyingi za uongozi katika Chama tawala na Serikali ya Tanzania, na nje ya nchi bonyeza hapa usome mwenyewe. Na kwa baadhi ya mahojiano ambayo amekwisha yafanya bonyeza hapa na hapa usome, na hapa umsikilize.

Watanzania hatuna budi kushukuru kuwa na mwanamke jasiri na muwezaji wa mambo kama huyu. Gertrude Mongella ni mtu asiye tishika na ndio sababu hata dunia imeweza kumuona. Na baada ya kumfuatilia sana nimegundua jambo moja, si mtu anayekurupushwa na matokeo ya jambo, ni mtu anayeangalia nini kiini au chanzo cha jambo hilo. Mfano ni pale alipozungumzia ya umaskini na vita vya wenyewe kwa wenyewe katika bara la Afrika. Alisema kwamba" hebu tujiulize waafrika wengi wanaopigana utakuta wanamiliki silaha bora na za gharama mno, lakini mwafrika huyo huyo hana pesa hata ya kuweza kumnunulia mwanae kalamu!! Sasa hapo ujue lipo jambo.. ninani anayempa mwafrika huyu hizo silaha?? ..huyo ndiye wa kusakamwa kwani kama angekuwa na nia nzuri basi angempa kalamu au nyenzo za kufanyia kazi. Hebu usiache kumsikiliza katika kiungo nilichokuwekeeni hapo juu.

Zidumu fikra za Mama Mongella.