TAFUTA CHOCHOTE NDANI YA NKEMA

Monday 21 October 2013

WARIDI :TUNAIGA SANA UZUNGU KATIKA FILAMU ZETU MPAKA AIBU

Muigizaji wa siku nyingi Anna Costantine maarufu kama Waridi ambaye alitamba sana mwishoni mwa miaka ya tisini amesema kuwa maadili ya kitanzania na kiafrika yameshuka sana katika filamu zetu mpaka ni aibu kutokana na kuiga sana uzungu ambao hata wazungu wenyewe hawafanyi hasa kwa waigizaji wa kike. Akizungumza na Mwananchi Waridi alisema "maadili yameshuka, hatuendani na maadili ya mwafrika, wanaiga sana umagharibi, tunaiga mpaka inakuwa aibu, hata wazungu hawafanyi hivyo"

Waridi ambaye alitamba enzi hizo na kina Monalisa, JB, Bishanga na Aisha alipoulizwa kuwa anategemea kurudi lini katika filamu alisema "mwanzoni mwa mwaka ujao nitarejea, nimejipanga vilivyo, ni lazima nifanye vizuri, nina kipaji, nimesomea kazi hii(chuo cha sanaa Bagamoyo), pia nina karama ya uigizaji, nitarudi kwa kasi, nitatingisha kama awali"

                                                            
 
Waridi
 

No comments:

Post a Comment